Home » , , » HISTORIA YA VITA KUU KWA UPANDE WA AFRIKA MASHARIKI....

HISTORIA YA VITA KUU KWA UPANDE WA AFRIKA MASHARIKI....


Dar es Salaam. Imeelezwa kuwa bomu la kwanza kurushwa kwenye Vita ya Kwanza ya Dunia (WWI) kwa upande wa Afrika Mashariki lilitupwa katika Bandari ya Dar es Salaam.
Bomu hilo lililokusudiwa kuharibu mfumo wa mawasiliano bandarini, lilirushwa kutoka kwenye meli ya Waingereza iliyojulikana kama Astrea siku ya nne tangu kuanza kwa vita hivyo vilivyoua watu milioni 16 duniani kote.
Akizungumza nyumbani kwa Balozi wa Uingereza nchini, jijini hapa juzi, wakati wa kuazimisha miaka 100 ya WWI Afrika Mashariki, Mratibu wa Taasisi ya Great War in Africa, Dk Anne Samson alisema kuwa baadhi ya watu hawafahamu kuwa harakati za vita hivyo zilifanyika Tanganyika.
“Dar es Salaam ilipigwa bomu kutoka baharini Agosti 8, 1914 na wiki moja baadaye, Agosti 15, 1914 Jeshi la Ujerumani likiwa na askari 200 liliivamia Kenya katika mpaka wa Holili na Taveta wakati huo ikitawaliwa na Uingereza.

TOA MAONI YAKO HAPA

 
Support : Copyright © 2011. HABARILINE - All Rights Reserved