Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts

UCHAWA WASADIKIWA KUWA CHANZO CHA AJALI NA VIFO KWA WAIMBAJI WA INJILI....HABARI KAILI IHAPA


Gladness Mallya na Chande Abdallah KUTOKANA na ajali na vifo kwa muziki wa Injili vilivyotokea hivi karibuni, imedaiwa kuwa baadhi vimetokana na uchawi.Baada ya kuzagaa kwa habari hizo, mapaparazi wetu walimtafuta Rais wa Chama cha Muziki wa Injili, Addo Novemba ambapo alikiri kuwa kweli uchawi upo na unahusika.
Rais wa Chama cha Muziki wa Injili, Addo Novemba.
“Kwenye msafara wa mamba hata kenge wapo, hili la uchawi silikatai kwani hata kwenye vitabu vya dini limetajwa, kwa hiyo watu wafahamu kwamba tuna vita kali.
“Hata mimi ninasikia kuna baadhi ya waimba Injili na wachungaji wanaoenda Nigeria kwa ajili ya kuchukua nguvu za kishirikina lakini tunaendelea kuomba tunaamini Mungu anatupigania,” alisema Addo.
Mwanamuziki wa nyimbo za Injili, Bahati Bukuku.
Baadhi ya waimbaji waliofariki hivi karibuni ni pamoja na Deborah John Said (Juni 20), Egla Bavuma (Julai 22), Orida Njole (Julai 12) na Mandilindi William (Julai 15). Waliopata ajali ni Edson Mwasabwite na Bahati Bukuku ambao wote wanaendelea vizuri na matibabu,

HISTORIA YA VITA KUU KWA UPANDE WA AFRIKA MASHARIKI....


Dar es Salaam. Imeelezwa kuwa bomu la kwanza kurushwa kwenye Vita ya Kwanza ya Dunia (WWI) kwa upande wa Afrika Mashariki lilitupwa katika Bandari ya Dar es Salaam.
Bomu hilo lililokusudiwa kuharibu mfumo wa mawasiliano bandarini, lilirushwa kutoka kwenye meli ya Waingereza iliyojulikana kama Astrea siku ya nne tangu kuanza kwa vita hivyo vilivyoua watu milioni 16 duniani kote.
Akizungumza nyumbani kwa Balozi wa Uingereza nchini, jijini hapa juzi, wakati wa kuazimisha miaka 100 ya WWI Afrika Mashariki, Mratibu wa Taasisi ya Great War in Africa, Dk Anne Samson alisema kuwa baadhi ya watu hawafahamu kuwa harakati za vita hivyo zilifanyika Tanganyika.
“Dar es Salaam ilipigwa bomu kutoka baharini Agosti 8, 1914 na wiki moja baadaye, Agosti 15, 1914 Jeshi la Ujerumani likiwa na askari 200 liliivamia Kenya katika mpaka wa Holili na Taveta wakati huo ikitawaliwa na Uingereza.

WAASI WA M23 WASALITI AMRI NA KUDAI MAZUNGUMZO NA SERIKALI .NI BAADA YA HIKI KITENDO HAPA....

Wanajeshi wa serikali katika Jmauhuri ya kidemokrasi ya Congo, wanashambulia ngome ya mwisho ya waasi wa M23 katika maeneo ya milimani ,msituni Mashariki mwa nchi.
Mamia ya wakimbizi wanatoroka vita karibu na mpaka wa Mashariki mwa Congo na kuingia nchini Uganda.


















Viongozi wa kundi hilo la M23 walitoa wito kwa wapiganaji wao kusitisha vita na kuruhusu mazungumzo ya amani na serikali.
Kiongozi wa wapiganaji hao Mashariki mwa nchi ametangaza kuwa watasitisha mapigano katika vita vyao na jeshi la serikali.
Bertrand Bisimwa alisema kwenye taarifa kwamba anawasihi wapiganaji wote haraka waache uhasama na wanajeshi, ili kuwezesha mazungumzo ya amani kuendelea.
Wanajeshi wa serikali, wakisaidiwa na kikosi cha kuweka amani cha Umoja wa Mataifa, hivi karibuni wamewasukuma nyuma wapiganaji na kuwatoa katika ngome zao nchini.

MKE WAMTU SIMWENZIO:SHABARO ANUSURIKA KUTOWEKA DUNIANI BAADA YA KIPIGO CHA MBWA MWIZI KUMPATA.HEBU TAZAMA ILIVYOKUA

KIJANA mmoja mtanashati ‘Sharobaro’ ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja juzikati alijikuta akichezea kichapo cha mbwa mwizi kisa kikidaiwa kuwa ni mke wa mtu.


Usione vyaelea: Sharobaro (katikati) akilia baada ya kuchezea kichapo kwa kukutwa na mke wa mtu.
 Tukio hilo lilijiri saa saba usiku mwishoni mwa wiki iliyopita, Chalinze mkoani Pwani ambapo mapaparazi wetu walikwenda kwa ajili ya uzinduzi wa kundi jipya la sanaa liitwalo 3 Ways.
 Wakati shamrashamra zikiendelea, ghafla liliibuka timbwili na katika kufuatilia ilibainika sharobaro anayeishi eneo hilo alikuwa akila kipigo kutoka kwa mwanaume mmoja akimtuhumu kuwa alimkuta akiwa amekaa chobingo kihasarahasara na mkewe.

Mke wa mtu sumu: Sharobaro hoi baada ya kipigo.
 Licha ya baadhi ya wasanii kujaribu kuingilia kati ugomvi huo, jamaa huyo aliendelea kushusha kichapo hadi pale watu walipomtolea uvivu na kumzuia asije akasababisha mauaji.
 “Unajifanya sharobaro halafu unazengea wake za watu, sasa wee umeipata fresh na huyo mwenzako akirudi nyumbani naye
atakiona,
” alisikika akisema mwanaume huyo huku akionekana kufura.

 Kufuatia kichapo hicho, sharobaro huyo alijikuta akiangua kilio huku akilalama kuwa mwanamke huyo amemponza na kumharibia siku yake.
 

Kilio: Sharobaro akizidi kububujikwa na machozi baada ya kipondo kutoka kwa mwenye mali.
 Wakizungumzia tukio hilo, baadhi ya mashuhuda walisema, kipigo alichopata kijana huyo ni fundisho kwa masharobaro wengine ambao wamekuwa na uhusiano wa karibu na wake za watu.
 “Unajua hawa vijana hii ndiyo dawa yao, wanajisahau sana. Yaani anajua kabisa fulani ni mke wa mtu lakini anajiweka, sasa kwa kipigo hiki atakuwa fundisho,” alisema baba mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Baba Zulfa.
 Aidha, wengine walimtetea kijana huyo na kudai kuwa mwanamke huyo ndiye anayestahili kulaumiwa kwa kukubali kukaa gizani na kijana huyo wakati akijua ni mke wa mtu.

WANAJESHI WA KENYA KDF WAMEISHAMBULIA KAMBI YA MAFUNZO YA AL-SHABAAB NA KUUWA WATU 300:



The Kenya Defence Forces (KDF) warplanes have bombed and destroyed Al-Shabaab training camp in Somalia in retaliation for September’s terror attack on Westgate Mall, where 70 people were killed and scores wounded by terrorists.

 
Speaking yesterday, KDF Spokesman, Colonel Cyrus Oguna, noted that the Kenyan drone strike on Thursday killed several Al-Shabaab terrorists destroying the training camp where Al-Shabaab organized the Westgate Mall attack.
 
“We have been monitoring this area for some time and we moved in when we got the green light. This is the same area where Al-Shabaab attackers at Westgate did their training”, said Oguna.
 
The camp had over 300 Al-Shabaab terrorist fighters many of who were killed and only a few survived with serious injuries in the attack.
 
However, the Al-Shabaab denied there having been any attack on their training camp, saying it was mere propaganda by KDF.
 
“No military of ours in Somalia was air struck or attacked”, said a senior Al-Shabaab fighter.
 
 
The Kenyan DAILY POST

DK SLAA APONDA MFUMO MPYA WA UFAULU.....HOJA ZAKE HIZI HAPA


SIKU tatu baada ya serikali kutangaza mfumo mpya wa madaraja ya ufaulu, licha ya kupingwa na wengi, kitendo hicho pia kimemhuzunisha Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.
Akizungumza  jana, Dk. Slaa alisema:  “Kwa kubadili mfumo wa maksi serikali sasa bila huruma imeamua kwa makusudi kabisa kuua ubora wa elimu nchini, ni kweli kwa kupanua wigo wa kufaulu serikali haitalaumiwa kwa akili ya kawaida, itaonekana  wamefaulu wote, lakini elimu haitawasaidia watoto wenyewe, haitawasaidia wazazi wenyewe,  na haitasaidia taifa letu.

 Tutapataje madaktari bora, tutapataje wanasayansi, walimu au wahandisi bora?  Mabadiliko yanahitajika kusaidia taifa hili lisizikwe na watu wasio na huruma.”
 

Kwa upande wake, Dk. George Kahangwa, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akizungumza kupitia kipindi cha ‘Tuongee’ kinachorushwa na Star TV,  alisema  hatua ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa Sifuni Mchome, kutangaza mageuzi hayo ni kuonesha ni jinsi gani serikali  imeshindwa kutatua mzizi  wa tatizo la elimu nchini na baadala yake inatapatapa kwa kuja na sera iliyoiacha kuitumia toka mwaka 1995 iliyotumia alama hiyo ya 50 kwa 50  kwa Tanzania Bara na 40 kwa 60, kwa Visiwani Zanzibar ambapo safari hii imeamua kuitumia tena na kuiweka wazi.
Dk. Kahangwa alisema serikali licha ya kutoa tamko la kubadilisha daraja jipya huku ikikiri kuwa ilikuwa ikitoa alama za kuanzia 75 hadi 100 ndio ufaulu wa alama ‘A’ na daraja la kwanza, pasipo kuiweka wazi kwa muda mrefu, sasa wameamua kuiweka wazi, huku ni kuwaada Watanzania kwa kutumia sera ambayo hazitekelezeki.
“Hili ni janga la elimu, huko nyuma waliondoa ‘sifuri’ kwenye ufaulu na kuweka ‘feli’, leo hii wanakuja tena na kuongezea daraja la tano na kuita ‘ufaulu hafifu au ufaulu usioridhisha’, huku ni kucheza na masuala ya msingi katika taifa. Kuja mbele za umma na kutangaza tena juu ya sera hiyo waliyoiacha kwa muda pasipokuitumia ni jinsi gani sera hiyo haitekelezeki tena,” alisema Dk. Kahangwa.
Dk. Kahangwa amewaomba Watanzania na wadau wa habari nchini kujitokeza kuwahoji wadau wa elimu kama walishirikishwa kwenye kupitishwa kwa mabadiliko hayo.
Dk. Kahangwa alisema  hivi karibuni kuna shirika lilifanya utafiti wa shule za sekondari 100 ambapo shule nne tu ndizo zinahesabika kama shule bora huku 96 zikihesabika kama makambi ya shule.
Hata hivyo, Mhariri Mtendaji wa gazeti la Tanzania Daima, Ansbert Ngurumo, aliyekuwapo kwenye mahojiano hayo alifananisha kitendo cha serikali kupanga madaraja hayo kuwa ni sawa na kupanua magoli ya uwanja ili kila mchezaji afunge, huku akiitaka serikali iwaombe radhi wananchi kwa kuwa ilianza kutumia mfumo huo bila kuwaarifu.
Naye Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Mwanza, Edwin Soko, alisema mabadiliko haya yaliyolenga kuongeza idadi ya wahitimu bila kuangalia uzoefu, yamesababisha taifa kukosa falsafa na Dira ya Taifa.

INASIKITSHA:HIKI NDICHO WANACHOFANYA MASTAA WA BONGO MOVIE WAKIWA KAMBINI,DUUU


KINACHOONEKANA kwa sasa Bongo ni ugumu wa serikali kupambana na vita dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi baada ya jamii kushindwa kubadilika na kuona ugonjwa huo ni wa kawaida kama ilivyo kukohoa au kichwa kugonga.
Hilo limedhihirika baada ya juzi chanzo chetu cha habari kupasha kwamba, baadhi ya wafanyabiashara na wabunge wameingia ‘kazi’ ya kuwanasa mastaa wa kike Bongo, hasa waigizaji wa filamu.


Kwa mujibu wa chanzo hicho, wafanyabiashara maarufu wa jijini Dar na baadhi ya waheshimiwa wabunge wamekuwa wakiwaibukia mastaa wanapokuwa kambini wakirekodi filamu na kuwahonga fedha nyingi sanjari na kuwanunulia magari ya kifahari ya kutembelea.


Inadaiwa wanachofanya baadhi ya mastaa, hasa wakiwa kambini, hupiga picha chafu wakiamini zina mvuto na kuzitundika BBM kwenye simu zao ambapo wafanyabiashara na wabunge hao wanapoziona huweweseka na kuanza msako wa kuwapata.
Chanzo kilisema: “Zamani mapedeshee ndiyo walikuwa wanaongoza kwa kuwachukua mastaa wa kike kwa kutumia picha za mitandaoni na kwenye magazeti, siku hizi mastaa wenyewe wamewashtukia, hawawataki mapedeshee, wanasema fedha zao ni za msimu.


“Siku hizi mastaa wakiwa kambini hupiga picha za hasarahasara na kuzitupia BBM, wafanyabiashara na wabunge wakiziona wanakimbilia kupanga foleni kwenye mahoteli ambayo mastaa hao wamepiga kambi.”


Aidha, chanzo kikasema kuwa baadhi ya wafanyabiashara huhonga kuanzia shilingi 1,000,000 hadi 5,000,000 kama staa ana jina kubwa.


“Kama staa ana jina kubwa, anaweza kuhongwa kuanzia milioni moja hadi tano, kama ni supastaa kama Wema, Wolper, Odama, Rose Ndauka hawa wanaweza kuhongwa hata magari ya kifahari,”kilisema chanzo hicho.



Chanzo kikasema kuwa, mbaya zaidi wanaume hao wamekuwa wakigoma kufanya mapenzi kwa kutumia kinga (kondom) kwa madai kwamba, hawawezi kuhonga pesa nyingi halafu kitandani wakatumia kondom kwani wanakosa raha.
“Kinachouma zaidi ni kwamba, hao wanaume wakiwachukua mastaa hadi chumbani wanakataa kutumia kondom, madai yao pesa wanazohonga ni ndefu (nyingi) kwa hiyo ni afadhali wafaidi, wanasahau kwamba Ukimwi upo.


“Kwa sababu ya tamaa ya pesa, dada zetu (mastaa) wanashindwa kuwa na msimamo wa kutumia kondom. Anaweza kukataa sana, lakini mheshimiwa anaahidi kumnunulia gari, hapo ndipo masharti yanalegezwa,”kilisema chanzo.



Chanzo kikasema kumekuwa na vilio na kusaga meno kwa baadhi ya mastaa kwani wanaponunuliwa magari, kadi zinakaa kwa wanaume hao, baadaye wanawanyang’anya.


“Mbaya zaidi, wapo mastaa waliwahi kushawishika na kutoa penzi bila kinga kwa ahadi ya kununuliwa gari, waliponunuliwa hawakupewa kadi ya kumiliki, baadaye wakanyang’anywa,” chanzo kilitoboa.


Baadhi ya mastaa waliozungumza na paparazi wetu walikiri kuwepo kwa wanaume wenye tabia hiyo, lakini kila mmoja akasema yeye haijamtokea.
Wolper:
 “Ni kweli, wapo wanaume wanabembeleza sana kutotumia kondom na kuahidi fedha au gari, lakini kama staa anakubaliana na ombi hilo ni kujiangamiza, Ukimwi unaua. Ila mimi sijawahi kukutana na mwanume wa hivyo, kwanza nilishasema ndani ya gari natembea na kondom.”


Jack wa Chuz: “Wewee, uamuzi wa kufanya hivyo ni wa mtu mwenyewe na umri wangu huu nikubali kufanya mapenzi bila kinga kwa sababu ya gari? Kwani gari kitu gani bwana.”


Nisha: “Mh! Nimewahi kusikia kuna wasanii waliingia kwenye mtego huo na sasa wanajuta maana hawana uhakika na afya zao, kwenda kupima wanaogopa, magari walishanyang’anywa, mimi aku!”


Flora Mvungi“Mimi siwezi kusema kitu maana nina wangu, kama ni gari au pesa ananipa yeye, pole yao ambao hawajajipanga hadi leo.”


Aidha, chanzo kilisema kuwa, maeneo hatari ya kufanyika kwa michezo hiyo ni hoteli kubwa ambazo wasanii hupiga kambi kwa ajili ya kurekodi filamu.

BUNGENI:MH ZITTO NA LEMA WAINGIA KATIKA VITA YA MANENO,CHANZO CHA MKASA HIKI HAP

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu hali ya vurugu zinazoendelea Mtwara katika sakata la mradi Gesi asilia kuja Dar es Salaam.PICHA NA VENANCE NESTORY

Dodoma: Wabunge Wawili Maarufu wa Chadema, Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini) na Godbless Lema (Arusha Mjini) wameingia katika vita ya maneno ambayo chanzo chake ni kauli ya Lema aliyotoa katika kikao cha wabunge (briefing) kilichofanyika mjini Dodoma Jumanne wiki hii.
Lema akizungumza katika kikao hicho, anadaiwa kutoa maneno ambayo yalitafsiriwa na wabunge wengi kuwa yalikuwa yakimlenga Zitto kuhusu hatua yake ya kukataa posho na kumtuhumu kwamba ana ukwasi ambao unapaswa kuhojiwa.
Gazeti hili lilimtafuta Lema likirejea taarifa iliyotolewa na Zitto akilalamika kwamba Lema alimshambulia katika kikao hicho cha wabunge wote na kwamba alikuwa akimlenga yeye.
Lema, hata hivyo, alikiri kuzungumzia suala hilo akisema:
“Mimi sikumtaja mtu, kwahiyo kama kuna mtu analalamika hilo ni suala jingine, ila mimi nilimaanisha nilichokisema”.
Hata hivyo, Zitto alieleza kuwa msimamo wa Lema ulikuwa unapingana na wabunge wengine wa Chadema, ambao waliwahi kupendekeza kuwa posho zifutwe.
Zitto alisema kuwa yeye mwenyewe, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika waliwahi kupendekeza kuwa posho zifutwe.
“Mimi sipokei posho kabisa, posho za vikao na ndiye mbunge pekee ambaye hapokei posho ya vikao tangu mwaka 2011,” aliongeza Zitto, ambaye anahudhuria mkutano unaozungumzia uendeshaji wa Serikali kwa uwazi huko London, Uingereza.
Zitto alisema malipo ya wabunge mpaka sasa ni makubwa sana ukilinganisha na hali ya wananchi wakati Serikali ikishindwa kulipa vizuri walimu na wauguzi.
“Hatuwezi sisi kama wabunge kuanza kulilia posho, wakati wananchi wetu hawana maji, hatuwezi kulilia posho. Mbunge anayetaka posho zaidi akafanye kazi nyingine na awaachie wanaoweza kuwakilisha watu waendelee,” alisema Zitto.
Lema, hata hivyo, alisema kwamba katika mkutano huo aliweka bayana kwamba umasikini siyo uzalendo na kusisitiza kuwa wabunge wanapaswa kuwa na maslahi bora na wakati huohuo wana wajibu wa kuwatetea watumishi wengine wa umma.
“Nilisema huwezi kuzuia taasisi moja kupewa maslahi bora eti tu kwa sababu watumishi wengine hawalipwi vizuri, ni haki wabunge kulipwa vizuri na wakati huo wapiganie maslahi ya watumishi wengine,” alisema Lema na kuongeza:
“Kwahiyo nikasisitiza kwamba nawashangaa wale ambao wanakataa posho ya Sh80,000 na ukienda kuchunguza wanakatwa fedha zote kutokana na mikopo waliyochukua, lakini bado wakija sehemu kama Arusha wanalala kwenye hoteli ya gharama kubwa kati ya Dola za Marekani 150 na 600”.
Alisema katika mazingira hayo kunakuwapo maswali mengi yasiyokuwa na majibu na kwamba mbunge wa aina hiyo alitakiwa anapokuwa katika mji wowote nchini aishi katika hoteli yenye thamani kati ya Sh20,000, 30,000 na hata Sh50,000.
“Kwa hiyo ikiwa unakataa posho ya Sh80,000 halafu unalala chumba cha Dola 600 hustahili kupata credibility (sifa) stahili, ni unafiki tu na kutafuta sifa za kipuuzi,”alisema Lema.
Alisisitiza kwamba wabunge wa Tanzania hawalipwi ipasavyo na kwamba kudai malipo ya ziada hakuwaondolei wajibu wao wa kuwatetea watumishi wengine wa umma ambao pia malipo yao ni kidogo.
“Kuna hatari ya kuona kwamba Sh80,000 au Sh200,000 ni fedha nyingi, ni kwamba kama sisi wabunge tutalipwa Sh50,000 basi maana yake ni kwamba walimu au polisi tutaridhika wakilipwa hata Sh10,000,”alisema
Mwananchi

IRENE PAULO:LUGHA INA MCHANGO MKUMBWA KATIKA MAFANIKIO YA FILAMU KISASA KAMILI HIKI HAPA

Mwigizaji huyo ambaye hivi karibuni aliingia mzigoni kutengeneza filamu na staa kutoka Ghana, Van Vicker, anasema lugha ina mchango mkubwa katika mafanikio ya filamu. 
Mbali ya hilo, Irene ametumia wasaa aliopewa na gazeti hili kuwaasa Watanzania wakiwamo wasanii wenzake kwamba wawekeze kwenye suala la elimu la hususani lugha ya Kiingereza akisema ndiyo kikwazo kimojawapo kwa baadhi ya vijana kutopata ajira.
IRENE Paul, staa aliyewahi kutamba katika filamu za Kalunde, Saturday Morning, Kibajaji, Love & Power, Handsome wa Kijiji na nyinginezo nyingi, amesema ndoto ya filamu za Tanzania kutamba Afrika haitatimia kama waigizaji wake wataendelea kutumia lugha ya Kiswahili tu.
Mwigizaji huyo ambaye hivi karibuni aliingia mzigoni kutengeneza filamu na staa kutoka Ghana, Van Vicker, anasema lugha ina mchango mkubwa katika mafanikio ya filamu.
“Sitaki kusema watu waache kuigiza filamu za Kiswahili, ninajua kwamba tuna wateja wengi Bongo na pia ni wajibu wetu kuhakikisha lugha yetu inakua,” alisema.
“Lakini hatupaswi kuufumbia macho ukweli kuwa Kiingereza ndio lugha itakayotupaisha kimataifa.”
Mbali ya hilo, Irene ametumia wasaa aliopewa na gazeti hili kuwaasa Watanzania wakiwamo wasanii wenzake kwamba wawekeze kwenye suala la elimu la hususani lugha ya Kiingereza akisema ndiyo kikwazo kimojawapo kwa baadhi ya vijana kutopata ajira.
“Sasa hivi baadhi ya ofisi zetu zimetawaliwa na watu kutoka nchi za jirani, hata sisi wasanii baadhi yetu tunashindwa kuvuka mipaka huku lugha hiyo (Kiingereza) ikiwa ni kikwazo,” anasema na kuongeza.
“Ni wakati wetu Watanzania kujikita katika suala hili, pia hata kwa wasanii wenzangu. Wenzetu wa Nigeria, Ghana na kwingineko wanatamani kufanya kazi na sisi, lakini wakijaribu kuangalia filamu zetu na lugha tunayoitumia wanapata wakati mgumu japokuwa ni lugha ya taifa.”
Akizungumzia suala la waigizaji kugeukia kazi ya kuongoza filamu, Irene, anasema kwamba kamwe hawezi kuwa mwongozaji wa filamu kama ilivyo kwa wasanii wengi wenye majina, badala yake kazi hiyo anawaachia watu wengine ili kila kazi anayoifanya iwe na umakini na utaalamu zaidi.
Kuna tabia imejengeka kwa baadhi ya wasanii wa tasnia hiyo kujivika madaraka mengi yakiwamo ya mwongozaji, mtayarishaji na mwigizaji katika filamu moja.
Anasema hali hiyo inasababisha umakini katika utayarishaji wa filamu kupungua.
“Mimi nimeamua kuwa chachu ya mabadiliko, nimeona bora nimuite mtaalamu wa kuongoza afanye kazi yake, mtayarishaji naye afanye kazi yake ili mwisho wa siku, macho na mawazo ya wengi yaweze kuzaa kitu ambacho kitasaidia kusukuma ubora wa kazi zetu,” alisema.

WANAWAKE:FAHAMU MAZOEZI YA KUFANYA UKIWA NA UJAUZITO,


Kufanya mazoezi wakati wa ujauzito kuna umuhimu mkubwa kwa afya ya mama mjamzito mwenyewe na mtoto wake ambaye bado hajazaliwa. Wanawake wengi wanatambua umuhimu wa kula lishe bora, kuhudhuria kliniki, kuacha kuvuta sigara na kunywa pombe wakati wakiwa na mimba. Lakini si wanawake wengi wanaoelewa umuhimu wa kutumia muda wao kufanya mazoezi wakati wa ujauzito. Mazoezi yana umuhimu mkubwa kiafya wakati wa ujauzito kama ilivyo kabla ya ujauzito. Kufanya mazoezi wakati unapobeba mimba kunaleta faida kubwa wakati wa kujifungua. Wakati wa ujauzito ni muhimu kudhibiti ongezeko la uzito wa mama. Kwa kujishughulisha mama mjamzito na kuwa na harakati humsaidia awe na afya bora na kumsaidia aweze kupitisha kipindi cha uchungu na kujifungua kwa urahisi zaidi. Zaidi ya kumsaidia mama asiongeze uzito mkubwa wakati wa mimba, kufanya mazoezi humsaidia mama pia kurejea katika uzito wake wa kawaida kwa urahisi baada ya kujifungua kwa kawaida au kwa uparesheni. Kwa ujumla mama mjamzito kama ambayo anavyoshauri kula chakula bora na kuwa na afya nzuri wakati wa ujauzito, hivyo hivyo hushauriwa pia kuzingatia suala zima la kufanya mazoezi na kuchunga mwili wake usiongeze uzito mkubwa. Pia kufanya mazoezi huufanya mwili utoe mada ya endorphins, ambayo husaidia kumfanya mama asipate matatizo ya kifikra na msongamano wa mawazo (emotional stress na depression).

Zifuatazo ni faida anazozipata mama mjamzito iwapo atafanya mazoezi:


1. Mazoezi hupunguza maumivu ya kichwa, kukosa choo na kuvimba mwili. 


2. Mazoezi huongeza nguvu na kuupa mwili stamina.


3. Mazoezi hukufanya ujisikie vizuri na kukufanya uwe katika hali ya furaha.


4. Mazoezi hupunguza maumivu ya mgongo na huimarisha mifupa ya mgongo, makalio na mapaja na kuifanya iwe na uwezo wa kuvumulia vyema uzito wa mimba.


5. Mazoezi husaidia huongeza mtiririko wa damu na hewa katika ngozi na kuifanya ngozi yako ionekane nzuri.


6. Mazoezi hutayarisha mwili wako uwe tayari kwa ajili ya kuhisi uchungu kwa muda mfupi na kujifungua kwa urahisi. 


7. Mazoezi hufanya mwili wako urudi upesi katika muonekano wake wa kawaida baada ya kujifungua. 


8. Mazoezi humsaidia mama mjamzito apate usingizi kwa wepesi na kulala vyema.
 


Hata hivyo mama majamzito anashauriwa kabla ya kuanza kufanya mazoezi apate ushauri wa daktari na kuhakikisha kuwa hana matatizo ambayo kwa kufanya mazoezi pengine yakahatarisha mimba yake. Kwa wale waliokuwa wakifanya mazoezi kabla ya kubeba mimba wanashauriwa kuendelea na mazoezi yao lakini kwa kuwa waangalifu na kwa kiwango kidogo. Lakini kwa wale ambao walikuwa hawafanyi mazoezi hawaruhusiwi kufanya aina zote za mazoezi wakati wa ujauzito. Mazoezi kama vile kuogelea (kwa wale anaojua kuogelea), kutembea na yoga ni miongoni mwa mazoezi yanayoshauriwa wakati wa ujauzito. La muhimu ni mama mjamzito kutokaa tu na kujiepusha na uvivu na pengine kwa kufanya shughuli zake tu za kawaida ambazo mama huwa anazifanya nyumbani kila siku ikawa inatosha kuwa mazoezi yake na akaongeza kwa kutembea kidogo ( walking) kila jioni. Kutembea ni mazoezi salama na rahisi kwa kila mama mjamzito na yanayojulikana na kila mtu na kuweza kufanywa mahala popote. Ni bora kama unaweza fanya mazoezi na mwenza wako, rafiki au hata ndugu na jamaa yako ili uweze kufurahia zaidi mazoezi hayo. La muhimu ni kufuata maelekezo ya daktari kwani si kila mama mjamzito anaruhusiwa kufanya mazoezi wakati wa ujauzito kutokana na sababu tofauti. Baadhi ya mazoezi ambayo yana madhara kwa afya ya mama mjamzito na kwa mtoto hayaruhusiwi kabisa kufanywa wakati wa ujauzito. Mazoezi hayo ni kama vile mazoezi ya aerobic, ski, kupanda mawe, kupanda farasi na mengineyo kama hayo. Iwapo unaishi katika miji iliyoendelea basi unaweza kupata kwa urahisi vituo maalum kwa ajili ya kufanyia mazoezi mama wajawazito, na katika vituo hivyo kwa kawaida wakina mama wajawazito hukusanyika na kufanya mazoezi kwa pamoja. Lakini kama uko katika miji ambayo vituo hivyo hakuna usife moyo, na jitahidi kufanya mazoezi hayo peke yako huku ukishirikiana na familia yako.

MWANZA:MGANGA AKAMATWA NA KIGANJA CHA BINADAMU AKIWA KWENYE HARAKATI ZA KUKIUZA.MKASA KAMILI HUU HAPA


Mtu mmoja jijini Mwanza anadaiwa kukamatwa na kiganja cha mtu akiwa anajiandaa kumuuzia mteja kwa sh million 100.

Washukiwa walikamatwa  jana  karibia na uwanja wa ndege wa Mwanza  wakifanya  biashara  hiyo  haramu.... 
 Baada  ya  upekuzi  wa  kina, mteja  alikuwa  ana  milioni  100  na mganga alikutwa  na   kiganja cha  binadamu  ambacho kilikuwa  kibichi kikitoa damu.
Kiganja  hicho  kilikuwa  kimevishwa  tunguri  na nywele za binadamu.

INASIKITISHA:MZAZI AKOSA UTU,AMWADHIBU MWANAE KWA SILAHA ZA ULINZI KWA KOSA LA KUTOKWENDA SHULE HEBU TAZAMA HAPA

Victoria Mukama (10) akiwa hospitali ya rufaa mbeya baada ya kupigwa na baba yake mzazi sehemu mbali mbali za mwili wake akitumia vifaa vya ulinzi likiwemo Lungu.
Mwalimu wa zamu wa Shule ya Msingi Airport, Damali Obadia alisema tukio hilo la ajabu lilitokea majira ya saa mbili na nusu asubuhi ambapo akiwa ofisini alimuona mzazi huyo akiwa na mtoto huku akiendelea kumpiga wakielekea ofisini.
Mama mzazi wa binti huyo Teodora Paulo alisema yeye na mume wake hawakuwepo nyumbani ambapo baada ya kurejea kutoka Msibani majira ya asubuhi walimkuta binti yao hajaenda shule na walivyomuuliza sababu ya kutoenda shule alijibu alikuwa havioni viatu vyake.
majirani wa mtuhumiwa huyo walidai kuwa tabia ya Mwanaume huyo kufanya unyanyasaji inafichwa na mkewe ambaye anaonekana kuwa muoga wa kupigwa na mumewe na kuongeza kuwa anatabia ya kuandika makosa anayotendewa na mkewe.
Victoria Mukama (10) baada ya matibabu
KATIKA hali isiyokuwa ya Kawaida, Baba mmoja aliyejulikana kwa jina la Oscar Mukama mkazi wa Isengo Airport Jijini Mbeya amemjeruhi vibaya binti yake Victoria Mukama (10) kwa kumpiga sehemu mbali mbali za mwili wake akitumia vifaa vyake vya ulinzi likiwemo Lungu.
Kwa mujibu wa Mwalimu wa zamu wa Shule ya Msingi Airport, Damali Obadia alisema tukio hilo la ajabu lilitokea majira ya saa mbili na nusu asubuhi ambapo akiwa ofisini alimuona mzazi huyo akiwa na mtoto huku akiendelea kumpiga wakielekea ofisini.
Alisema mzazi huyo baada ya kufika walimu walimpokea na kumuuliza kwa nini anampiga kiasi hicho mtoto wake alijibu mtoto ni wa kwake mwenyewe na alizaa kwa manufaa yake hivyo haoni sababu ya kuulizwa kuhusu kipigo kwa mwanaye.
Aliongeza kuwa baada ya walimu kumweleza kuwa kitendo alichokifanya ni cha kinyama na hakipaswi kutendeka Mzazi huyo alitoa kisu na kuwatishia walimu ikiwa ni pamoja na kutoa matusi makali dhidi yao ambapo walimu walifanikiwa kumtuliza na kumuomba amwache mtoto ili walimu wamwadhibu.
Alisema baada ya mzee huyo kuondoka na kumwacha mtoto walimpigia simu mama wa mtoto ambaye baada ya kufika shule alizimia kutokana na hali aliyomkuta nayo mtoto wake ambapo Walimu walitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Mtaa kasha kwenda Polisi kuchukua Fomu namba tatu (PF3) kwa ajili ya matibabu.
Mama mzazi wa binti huyo Teodora Paulo alisema yeye na mume wake hawakuwepo nyumbani ambapo baada ya kurejea kutoka Msibani majira ya asubuhi walimkuta binti yao hajaenda shule na walivyomuuliza sababu ya kutoenda shule alijibu alikuwa havioni viatu vyake.
Alisema baada ya kumsaidia kutafuta na kutofanikiwa kuviona baba yake ambaye nayeb alikuwa amejiandaa kwa ajili ya kwenda kazini kwake anakofanya kazi ya Ulinzi alimwamuru mwanaye kuvaa sare za shule na kwenda naye hivyo hivyo kwa kile alichodai anampeleka shule.
Alisema alishikwa na butwaa hadi kupoteza fahamu baada ya kumkuta mtoto amejeruhiwa huku akiwa amepigiwa simu na mumewe kwamba aende shule kumchukua mtoto wake lakini hakujua kama amepigwa kiasi cha kumjeruhi mtoto sehemu mbali mbali za mwili wake.
Akizungumzia kisa cha kupigwa kwake baada ya kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya katika Chumba cha dharula, Victoria Mukama (10) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la nne katika Shule ya Msingi Airport alisema wakiwa njiani kuelekea shuleni alishangaa akianza kupigwa bila kuelezwa sababu ni nini.
Alisema alianza kupigwa tangu wanatoka nyumbani hadi wanafika shule iliyoumbali wa Mita 250 kutoka Nyumbani hadi Shuleni akitumia Virungu na fimbo huku akiwa ameshika kisu mkononi kwa ajili ya kuwatishia wanataka kumuokoa.
Kutokana na tukio hilo Jeshi la Polisi linaendelea kumtafuta Mtuhumiwa huyo wa unyanyasaji wa watoto baada ya kufunguliwa kwa jarada lenye namba MB/IR/9563/2013 katika kituo cha kati cha Polisi Mbeya.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Pambogo Esia Edward ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Shule hiyo alisema kitendo kilichofanywa na mtuhumiwa huyo hitendo hakipaswi kufumbiwa macho hivyo ni lazima sheria ichukue mkondo wake kwa kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa ndani ya jamii.
Aliongeza kuwa hajawahi kusikia mtuhumiwa huyo kama amewahi kujihusisha na ukatili wa namna hiyo na kuongeza kuwa huwa anatoa ushirikiano vizuri katika ngazi ya mtaa na kuhudhuria vikao mbali mbali vinavyoitishwa pamoja na kuchangia mada.
Nao majirani wa mtuhumiwa huyo walidai kuwa tabia ya Mwanaume huyo kufanya unyanyasaji inafichwa na mkewe ambaye anaonekana kuwa muoga wa kupigwa na mumewe na kuongeza kuwa anatabia ya kuandika makosa anayotendewa na mkewe.
Walisema awali amewahi kuoa mke na kuzaa nae watoto watatu lakini mkewe huyo alikimbia baada ya kuona tabia ya unyanyasaji imezidi kutoka kwa Mwanaume huyo aliyetajwa kuwa ni jamii ya watu wa Mosoma Mkoani Mara ambako tabia kandamizi dhidi ya wanawake na watoto bado zinafanyika.

TB JOSHUA ATABIRI MAKUBWA KWA MARAISI AFRIKA MASHARIKI,INASIKITISHA SANA..HEBU JIONEE


Yule Mchungaji Maarufu kutoka Nigeria Ambae hutabiri mambo mbalimbali na kweli yakatokea  TB Joshua leo ametoa utabiri mpya ambao unahusisha Africa Mashariki ...ameonyeshwa rais mmoja Africa Mashariki atatekwa na ameonyeshwa watu wakiwa club wanacheza then wanalipukiwa na nchi iyo ni jirani na Kenya, Angalizo, amesema siyo kenya tena,je itakuwa nchi gani? 

Misa ya jana jumapili ndo kasema, na amesema ataendelea kuomba ili jumatano na alhamisi ijayo aonyeshwe ni rais gani na nchi gani.


Jamani tuombe sana isiwe Tanzania

BERLIN:MNYAMA AITWAYE BEAR AMSHAMBULIA MWANAMKE MMOJA,TAZAMA LIVE ILIVYOKUA(VIDEO)

polar bear attacked This is a woman at Berlin Zoo  Friday afternoon Effective she Climbed a fence and jumped into icts habitat falling on feeding time, the police said Saturday. One adult  polar  bit her several times Effective she plunged into the moat, the police said. Zoo workers tossed rescue rings Toward  the woman  to hoist her out and distract  polar bears  swimming Florida, said Goerg Gebhard, a Berlin police officer. One at the point  the woman  fell back into the water and was grabbed by a  bear  before she was hoisted to safety Eventually. "They saved her life," Gebhard Told CNN.  The woman  was injured and was Severely Being Treated at a hospital, Police said.

HOW TO BE FREE FROM HEART BREAK,THE SOLUTION IS HERE,,,


A MUST READ:HOW TO be free from HEART BREAK
1. Forgive The Person That Hurt You: Forgiveness is the number one secret of recovering from heart break. When you truly forgive someone that had hurt you, it generate your own healing  Heart break comes as a result of disappointment or hurt from a love one. There are a lot people in marriage yet heartbroken. Most cases as a result of unfaithfulness from spouse.

It could really hurt when a spouse cheats on you. But Forgiveness is the only relief peel to be freed from hurts and heart break. Unforgiveness can hold you in a spot; it is like drinking poison and expects another person to get sick, it can hinder your access to God and your future. Unforgiveness or bitterness over a past hurt is telling yourself you do not need a future spouse or honeymoon.

A lot of people are not in a fruitful relationship today because of past hurts. They keep transferring their past experience to the very relationship they are into, at the end, they mess it up. They become over suspicious, careful and they refuse to trust, and without trust love had no foundation.
Love is the engine that drives every relationship to its destination. Forgive everyone that had hurt you in the past and treat every future relationship or spouse as a fresh person.

2 Learn To Let Go: there is a huge difference between forgiveness and letting go of your hurt. Until you let go of a bitter relationship, you will not see a better one. If a partner show you either in words or attitude that you are not appreciated, do not stay in such relationship. The earlier you let go and position yourself for another relationship, the faster you get healed. 
Every singles lady should know, when a man wants to choose a life partner, is like going to the market to purchase a product, He is like buyer and you are like the product. Every buyer wants to purchase a product that suit the purpose he or she is purchasing it for. Also buyers look out for products with added values. 
So when a man walks out on you to pick another woman, do not mourn over him for too long, rather improve your product “you” so that another buyer can come and purchase you. Stop praying over a dead relationship so your healing process can begin for another fruitful relationship. Learn to let go of the past and look forward to a brighter future. Stop blaming yourself for what you could have done right, it was not meant to be, he or she was your learning process so you can be perfect for your future partner. I want to encourage you, if any person wants to walk out of your life, let them walk, they are not part of you, a part of you will never leave you. Let go of your past so you can let loose of your honeymoon. Forget about it, a large percent of your Today’s mistake is for your tomorrow’s intake. 

3. Encourage Yourself: Encouraging yourself is very important to your healing process and also it helps to boost up your self-esteem. Always see yourself as God sees you. Do you know why God calls you god, because He had never created a brand like you before neither will there be any after you. That is who God is, no one before Him or will there be any after Him. Be conscious of the fact that you are a peculiar brand that will never be repeated in the history of the earth, any person that walks out of your life has lost a treasure. Encourage yourself and build up yourself-worth. People come after values, when you build good value in yourself, spouse will hunt for you.

4. Do Not Be In A Hurry To Enter Into Another Relationship: 
People often say, “The best way to overcome a heart break is to get into another relationship.” Sorry, that is the worse way to overcome a heart break because there will soon be another heart break. Always be careful not to let situations control your life, be in charge of situations. Take your time to go into another relationship, forget about the hurt but learn from it. Know where you missed it. Be sincere to know your share or contribution to the failed relationship then improve on it in your next possible relationship. Be careful not to make same mistake in your next relationship and try to be open.

A lot of people make the mistake of transferring their past experience to the very relationship they are into, at the end, they mess it up. They become over suspicious, careful and refuse to trust, and trust is the foundation of love. Love is the engine that drives every relationship. Forget about your past hurt, and treat every future relationship or spouse as a fresh person.

Every relationship is a new opportunity to sell yourself, do not shut down some of your good characters or qualities simply because the other person did not appreciate it. Make sure you are completely healed before thinking of another relationship.

5. Know Every Step Back Is A Preparation For A Step Forward: I read a story of a lady that was in a relationship with a guy; he called her to say he no longer feel anything for her in the presence of his friends and said it was over. She begged him kneeling for about 2 hours yet he refused to even look at her. In the middle of that scene her phone rang, she picked it up and there was a male voice, “I am Mr. X”. We dated while growing up. Before I go further, are you married?” She replied “no, but why?” He said, “thank God”. She replied, “What is it to thank God for? I am 34 years old and not yet married.” He proposed then and there. He added, “you do not need to give me a reply take your time and pray about it, I had informed my people, I even got your number from my younger brother”. She got up from her knees and walked out of her ‘EX’. As at the time I read this story he had flown to Nigeria from the States to file for her and they walked down the aisle on the April 13, 2013 in Maryland U.S.A. Yours may not exactly happen this way, but know any one that walked out of your life is pushing you forward to a better future. The best is yet to come. 
These secrets were given to me by God Almighty to share with you, as you practice them, your victory is sure.

……Judith Daniel-imagoro

VIGOGO WA CCM WALIOBAHATIKA KUPATA SHAHADA CHUO KIKUU HURIA,HAWA HAPA

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma katika Idara ya Itikadi na Uenezi CCM, Makao Makuu, Daniel Chongolo, akipongezana na Mjumbe wa NEC ya CCM, Asha Abdallah Juma baada ya wote kutuniwa shahada zao katika mahafali ya 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), yaliyofanyika jana, Oktoba 27, Bungo, Kibaha mkoa wa Pwani. Chongolo ametunukiwa shahada ya kwanza ya Mawasiliano ya Umma na Asha shahada ya Pili ya Biashara. Katikati ni Kada wa CCM, Rachel Kyala ambaye pia ametunukiwa shahada ya Mawasiliano ya umma.(Picha na Bashir Nkoromo)
2_a76fe.jpg
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha-Rose Migiro, akimpongeza Kada wa CCM, Asha Abdallah Juma, baada ya kumtunuku shahada ya pili ya Biashara, katika mahafali ya 25 ya chuo hicho, yaliyofanyika jana, Oktoba 27, 2013, Makao Makuu ya OUT, Bungo, Kibaha mkoa wa Pwani. Kushoto ni Makamnu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Tolly Mbwette. Asha ambaye sasa ni Mjumbe wa NEC CCM, amewahi kuwa Waziri katika serikali ya Mapinduzi Zanzibar na pia Katibu wa NEC, Oganaizesheni.

ARUSHA:VIONGOZI WA CHADEMA WAPEANA NAKOZI KWENYE MKUTANO WA MBOWE TAZAMA

Arusha. Mkutano wa Baraza la Uongozi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini juzi uligeuka ukumbi wa ngumi, baada ya Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba kushushiwa kipigo.

Mwigamba alishushiwa kipigo hicho na baadhi ya viongozi wenzake wa chama kwa madai ya usaliti na tayari amesimamishwa uongozi kwa muda usiojulikana.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas jana alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na viongozi hao wa Chadema kufikishana polisi.

 Alikutwa na zahama hiyo mbele ya viongozi wakuu wa Chadema Taifa, Mwenyekiti, Freeman Mbowe na mwasisi wa chama hicho, Edwin Mtei katika Hoteli ya Coridal Spring.

Viongozi hao wamekuwa wakifanya ziara za aina hiyo nchi nzima, kuimarisha chama na kujipanga kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani na uchaguzi mkuu ujao wa Rais na wabunge mwaka 2015.

Habari kutoka ndani ya mkutano huo zinaeleza kuwa hatua hiyo ilifuatia tuhuma kwamba Mwigamba alituma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Jamii Forums, unaodaiwa kukichafua chama hicho.

 Tukio hilo la aina yake lilitokea wakati viongozi wote wa juu wa chama hicho, wakiongozwa na Mbowe walipokuwa wakijadili mustakabali wa chama hicho, mkutano ambao ulihudhuriwa na wabunge karibu wote wa Chadema wa kanda hiyo.

 Hata hivyo, wakati mijadala ikiendelea baadhi ya viongozi wa chama hicho, akiwamo Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema walimtuhumu Mwigamba kutuma ujumbe kwenye mtandao huo, uliokuwa ukizungumzia ufisadi ndani ya chama hicho, wakidai alitaka Mwenyekiti Mbowe kukubali kuchunguzwa.  

Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana, Mwigamba alisema kuwa baada ya Lema kutoa tuhuma hizo aliungwa mkono na viongozi wengine na vijana waliokuwa wameimarisha ulinzi, kumvamia na kuanza kumpiga pamoja na kumnyang’anya kwa nguvu kompyuta mpakato (Laptop), aliyokuwa nayo, kisha kumpeleka Kituo Kikuu cha Polisi, mjini Arusha.  

“Wamenipiga sana na kuniweka ndani, ila nashukuru Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Arusha (OCCID),  alikuja na kunitoa saa 5:00 asubuhi,” alisema Mwigamba.

Alisema kuwa leo katika mkutano wake na waandishi wa habari ataeleza yote yaliyotokea na hatua atakazochukua, kwa kuwa yeye ni kiongozi wa juu wa chama. 


Hata hivyo, alieleza kwamba bado anashauriana na wanasheria wake kuona kama anaweza kuwachukulia hatua waliompinga.


Kauli ya polisi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema polisi wameona hakuna kosa la kisheria lililotokea hasa kutokana na malalamiko yaliyofikishwa kwao dhidi ya Mwigamba ya kukichafua chama kwenye mitandao.

 “Hili suala la mitandao ni kubwa na lina taratibu zake sasa kusema tu umechafuliwa na iwe kesi nadhani uchunguzi unahitajika kwao, sisi tumeona haya ni mambo yao wanaweza kuyamaliza wao ndiyo sababu tulimwachia, Mwigamba,” alisema Sabas.

Kosa analodaiwa kufanya Mwigamba

 Akizungumzia sakata hilo jana, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema kwamba Mwigamba alibainika kutuma ujumbe kwenye mtandao wa Jamii Forums uliokichafua chama hicho, akieleza haikuwa mara yake ya kwanza kwa kiongozi huyo kufanya hivyo na kwamba walikuwa wakimfuatilia kwa muda mrefu.

 “Kilichotokea ni hicho, vijana wa Red Brigade ndio waliomtoa ukumbini, baada ya kumbaini kukichafua chama, kwani laptop yake baada ya kuchunguzwa na wataalamu wetu walijiridhisha ni yeye ndiye aliyetuma ujumbe huo,” alisema Lema.

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa alitaja tuhuma zinazomkabili Mwigamba kuwa ni pamoja na kusema uongo, kupotosha taarifa za chama na kuchonganisha viongozi kupitia mtandao wa kijamii ya Jamii Forums.

Katika andiko lake kwenye mtandao, Mwigamba anadaiwa kuwatuhumu viongozi wa juu wa Chadema akiwamo Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk Wilbrod Slaa kuwa wamechakachua katiba ya chama hicho kuhusu ukomo wa nafasi za uongozi ili kujinufaisha binafsi.

Golugwa alisema kuwa baada ya kubanwa kwenye kikao, Mwigamba alikiri kuandika na kurusha taarifa hizo kwenye mitandao, lakini alipotakiwa kukabidhi kompyuta yake ili ichunguzwe na wataalamu wa mawasiliano wa chama hicho aligoma, hali iliyozua tafrani kati yake na walinzi wa chama hicho (Red Brigade), waliolazimika kutumia nguvu kumdhibiti.

Purukushani zilivyotokea

Habari zaidi zinaeleza kuwa katika harakati za kutaka kumnyang’anya Mwigamba kompyuta yake, mwenyekiti huyo wa Chadema mkoani Arusha alianza kushambuliwa na baadhi ya viongozi wa Chadema, kabla ya kufanikiwa kumdhibiti.


Zinaeleza kuwa katika tukio hilo kulitokea pia kurushiana maneno na matusi ya nguoni kati yake na viongozi wengine wa chama hicho akiwamo Lema.

Baadaye Lema aliliambia gazeti hili kwamba katika purukushani hizo Mwigamba alimrushia ngumi ambayo hata hivyo aliikwepa.

 Alisema kuwa wanakusudia kumfungulia kesi Mwigamba ya kukichafua chama chao katika mitandao ya kijamii.

 Hata hivyo, alisema kikao chao kiliendelea jana bila ya vurugu zozote na kuweka mikakati ya kushinda majimbo yote ya Kanda ya Kaskazini mwaka 2015 na kuchukua nchi katika uchaguzi huo ujao.

Adhabu kwa Mwigamba

Katika hatua nyingine Chadema, kimemsimamisha uongozi Mwigamba kwa tuhuma za kukisaliti, kukihujumu chama hicho na viongozi wake.

Akitangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari jijini Arusha jana, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Israel Natse alibainisha kuwa uamuzi wa kumsimamisha Mwigamba katika nyadhifa zote za uongozi ndani ya chama ulifikiwa na kikao cha Baraza la Uongozi wa Kanda ya Kaskazini kilichokutana juzi.

Alisema kuwa Mwigamba amesimamishwa kwa muda usiojulikana kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake na kuonya kuwa iwapo tuhuma zitathibitishwa, hatua nyingine za kinidhamu zitafuata kulingana na kanuni na katiba ya Chadema.

“Kwa sasa Mwigamba anatuhumiwa kuvunja sura ya kumi, kifungu cha 10.1 kifungu kidogo cha 8, 9 na 10 ya katiba ya Chadema inayozungumzia maadili ya uongozi,” alisema Natse.


Akifafanua zaidi alisema kuwa sura na vifungu hivyo vinakataza kiongozi wa chama hicho kutoa tuhuma dhidi ya viongozi wenzake bila kufuata vikao halali vya kikanuni na kikatiba.
 
Support : Copyright © 2011. HABARILINE - All Rights Reserved