Home » , , , » MH ZITTO KABWE AWASILISHA BARUA KWA KATIBU WA BUNGE INASEMA HIVI.

MH ZITTO KABWE AWASILISHA BARUA KWA KATIBU WA BUNGE INASEMA HIVI.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRCxBtynXOdrR-HnnZvPh-aG80__w3Q3-juBCZ6m31tcKDMIHt7Md1jRXOZLzGK96vZuQwD2ymWQXG3q5aMpM2bM7L4gpDn0EnNMLWRYWOveOOAf6YOjYH8W_SnTSMn3r571TslaSNiBAI/s640/Zitto-Kabwe.jpg

Mbunge wa Kigoma Kaskazini,Bw.Zitto Kabwe(CHADEM A),ameandika barua kwenda kwa Katibu wa Bunge akimkumbusha azimio la Bunge namba 9/2012 kuhusu Watanzania walioficha fedha nje ya nchi.
Katika barua hiyo,Bw.Zitt oalisema Mkutano wa Tisa wa Bunge la 10 uliofanyika mwezi Novemba 2012,kutokana na hoja binafsi ya mbunge,Bunge lil ipitisha Azimio la Serikali kufanya uchunguzi wa kina juu ya tuhuma za Watanzania kuficha mabilioni ya fedha za kigeni katika Benki za Ughaibuni hasa nchini Uswisi.Alisema Bunge liliagiza taarifa ya utekelezaji wa Azimio hilo iwe imewasilishwa bungeni kwenye Mkutano wa 11(Aprili,2013).Kutokana na kubadilishwa mfumo wa Bajeti ya Nchi,mkutano huo ulikuwa wa bajeti hivyo ilitaraji wa taarifa ya Serikali kuhusu utekelezaji wa azimio hilo,ingewasilishwa bungeni katika mkutano wa Agosti-Septemba 2013 lakini ilishindikana. " Pamoja na kwamba hoja ikishaamuliwa na Bunge ni hoja ya Bunge si ya mtoa hoja tena...nikiwa mdau mkubwa kwenye hoja hii, napata mashaka kwa nini Serikali imeshindwa kuwasilisha taarifa bungeni kwa mujibu wa Azimio la Bunge. "Kutowasilishwa taarifa hii,kunaleta wasiwasi miongoni mwa wananchi kuwa hoja husika imetupwa kapuni na Taifa halitapata ukweli kuhusu utoroshaji wa fedha za kigeni nje na kufichwa katika benki au kununua mali ughaibuni kama majumba,"alisema.Bw. Zitto aliliomba Bunge liitake Serikali iwa silishe taarifa hiyo juu ya utekelezaji wa Azimio la Bunge namba 9/2012 kuhusu Watanzania walioficha mabilioni nje kwenye mkutano wa Bunge uliopangwa kuanza Oktoba 29, mwaka huu
-majira

TOA MAONI YAKO HAPA

 
Support : Copyright © 2011. HABARILINE - All Rights Reserved