Showing posts with label MTUHUMIWA. Show all posts
Showing posts with label MTUHUMIWA. Show all posts

Msanii Masogange, mwenzake wapata dhamana Afrika Kusini...



Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kuzuia na Kudhibiti Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa 


Johannesburg. Watanzania Agness Masogange na Melisa Edward waliokamatwa kwa kutuhumiwa kubeba dawa za kulevya huko Afrika Kusini wameachiwa kwa dhamana.
Mkuu wa Kitengo cha Dawa za Kulevya Afrika Kusini, Kamishna Toto Mangaleni aliithibitishia Mwananchi jana kuwa watuhumiwa hao wameachiwa kwa dhamana,lakini wataendelea kubaki Afrika Kusini wakati kesi yao ikiendelea.
Mangaleni alisema wanawake hao ambao juzi pia walipanda kizimbani, walipata dhamana hiyo jana kutoka Mahakama Kuu ya Gauteng iliyoko eneo la Kempton Park jijini Johannesburg.
Hata hivyo, Kamishna Mangaleni alisema hawezi kuzungumzia zaidi kuhusu kesi hiyo kwa sababu hataki kuharibu uchunguzi ambao unaendelea dhidi ya Watanzania hao, ambao ni wasanii.
Marafiki wa karibu wa Masogange wanaoishi maeneo ya Midland Johannesburg ambao walikataa kunukuliwa majina yao, walithibitisha kuwa wanawake hao wameachiwa kwa dhamana.
“Ni kweli wameachiwa leo asubuhi. Lakini hatuwezi kuongelea kwa kina habari hizi kwa sababu hatutaki matatizo na polisi. Hii kesi bado inaendelea na wataendelea kubaki hapa hadi kesi yao itakapomalizika,” alisema mmoja wa marafiki zake.
Naye Masogange aliandika kwenye mtandao wa ‘Facebook’.
“Namshukuru Mungu nimeamini wewe ulikuwa pamoja na mimi katika maombi yangu na nashukuru kwa wote mliokuwa mkiniombea Mungu kapokea maombi yenu.”
Masogange na Melissa walikamatwa Julai 2 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg wakiwa wana mabegi sita makubwa ya dawa zinazoaminika kuwa ni `Crystal Methyl Amphetamine’.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kuzuia na Kudhibiti Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa aliiambia Mwananchi jijini Dar es Salaam kuwa alikuwa amepata taarifa za kuachiwa kwa wasichana hao, lakini alikuwa anawasiliana na watu wa Afrika Kusini ili kupata uhakika.
Nzowa, hata hivyo alilidokeza gazeti hili juzi kuwa kuna uwezekano wanawake hao wangepata dhamana au kufungwa kifungo chepesi kwani dawa walizokamatwa nazo ni kemikali zinazotumika kutengeneza dawa za aina tofauti kwa matumizi ya binadamu ingawa pia na dawa za kulevya.
Mamlaka yapinga uamuzi wa Mahakama
-mwananchi

MTUHUMIWA AJINYEA MAHAKAMANI WAKATI AKISOMEWA KIFUNGO CHA MIEZI 6 JELA JIJINI DAR...


 
 
Mtu mmoja amehukumiwa kifungu cha miezi sita jela katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Sokoine Drive kwa kosa la kujisaidia haja kubwa ndani ya Mahakama wakati akisomewa mashitaka. 

Adhabu hiyo ilitolewa papo hapo baada ya mshitakiwa Hassan Omary (25) kufanya kitendo hicho aliposomewa mashitaka mengine tofauti.
 
Hakimu William Mutaki ndiye aliyetoa hukumu hiyo. Wakati akisomewa mashitaka sanjari na washitakiwa wengine watatu ya kubughudhi abiria maeneo ya Kariakoo, Omary inadaiwa alitokwa haja kubwa.
 
Mwandishi alishuhudia mshitakiwa huyo akisafisha eneo la mahakamani alikochafua kabla ya kupelekwa jela. Wengine anaoshitakiwa nao katika kesi hiyo ni Mohamedi Mussa (20),Hassani Ramadhani (18),Shukuru Adison (26) na Ally Omary (28).

Mwendesha mashitaka wa serikali John kijumbe alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi William Mutaki kuwa washitakiwa walitenda kosa la kuwanyanyasa na kuwabugudhi abiria ,Septemba 18 ,mwaka huu Kariakoo, jijini Dar es Salaam. Washitakiwa wengine walirudishwa rumande hadi Oktoba 2,mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
 
Katika kesi nyingine, mshitakiwa Jacob Sasita (28) amehukumiwa kifungo cha mwezi mmoja baada ya kukiri kuwanyanyasa abiria .
 
Sasita alikuwa miongoni mwa washitakiwa saba waliofikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Washitakiwa wengine ni Ramadhani Juma (38),Abeid Ismail (25),Abuu Rajabu(25),Salimu Kijimbo (39),Ally Hassani (28),Josephb Chambo (29)na Fabiani Thomas (28) ambao walikana kutenda kosa baada ya kusomewa mashitaka.
 
Mbele ya Hakimu Mkazi Timoth Lyon, Mwendesha Mashitaka wa Serikari, Richard Magudi alidai watu hao walitenda kosa la kuwanyanyasa abiria katika kituo kikuu cha mabasai cha Ubungo ,kabla ya kukamatwa na askari polisi. Walirudishwa rumande hadi Oktoba 2 mwaka huu kesi itakapotajwa tena.

MAKUBWA: MTUHUMIWA ALOWESHA SURWALI PASIPOKUTARAJIA SHUHUDIA MWENYEWE



MTUHUMIWA, Manfred Adam anayekabiliwa na kesi ya kutishia kuua katika hali isiyotarajiwa amelimwaga kojo katika Mahakama ya Mwanzo na kuleta vurugu kubwa zilizosababisha kuvunjika kwa meza ya Mahakama ya Mwanzo ya Mazimbu mkoani  Morogoro mwanzoni mwa wiki hii.
 

Katika vurugu hizo zilizolazimisha shughuli za mahakama kusimama kwa muda wa saa mbili, askari wawili waliokuwepo eneo la tukio walishindwa kumdhibiti Manfred, kitendo kilichofanya kuitwa kwa wengine zaidi ambao waliweza kumtuliza mtuhumiwa huyo.

Hakimu Alisile Mwankejela aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo namba 322 ya mwaka 2013 pamoja na makarani wa mahakama hiyo walitimua mbio kuhofia kudhurika, mara tu baada ya vioja hivyo kuanza kufuatia kuahirishwa kwa kesi ya mtuhumiwa huyo ambayo itasomwa tena Septemba 24,    mwaka huu.

“Ni kweli tukio hilo limetokea baada ya kuhairisha kesi, mshitakiwa huyo alikojoa mahakamani na kufanya vurugu kubwa,” alisema hakimu huyo alipokutwa ofisini kwake.
Karani wa makahama hiyo, Kidawa Minangu alimwambia mwandishi wetu;


“Manfed asubuhi aliletwa hapa kwa ajili ya kesi yake, alipofika tuliita jina lake na aliingia mahakamani na kusomewa mashitaka yake, kesi ilipohairishwa cha ajabu alivua suruali na kukojoa hapa mahakamani, tuliwaita askari wawili wa hapa mahakamani walipomkamata alianza kupigana nao na kuvunja meza za mahakama ndipo tulipoamua kuomba msaada wa askari wengine ambao walifika na kumdhibiti.
 
Support : Copyright © 2011. HABARILINE - All Rights Reserved