Home » » MAONI JUU YA RASIMU YA KATIBA

MAONI JUU YA RASIMU YA KATIBA


Wapendwa wana CCM, itakumbukwa mnamo tarehe June 3, 2013 Tume ilitangaza Rasimu ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Hatua hii ya mwanzo ya kukamilika kwa katiba mpya ni sehemu ya kwanza ya kukamilika kwa katiba. Pia, ikumbukwe hatua ya pili ni kuwasilishwa rasimu ya pili kwenye Bunge la Katiba. Mwisho, kutakuwa na Rasimu ya tatu itakayofikishwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni.
Wana CCM, hatua hii ya pili ya tume ya katiba ni kwamba inajadiliwa katika mfumo wa mabaraza ya asasi na vyama vya siasa. Kwa kuzingatia kwamba chama cha mapinduzi ni taasisi muhimu na yenye maslahi makubwa katika upatikanaji wa katiba mpya.
Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ilikutana mjini Dodoma tarehe October 6,2013 ilitoa maamuzi ya kwamba uandaliwe ufafanuzi utakaorahisisha utoaji wa maoni utakaotumiwa na wana ccm katika kutoa maoni.
Madhumuin ya mpango huu ni kuwawezesha wana CCM kushiriki na kutoa maoni yao kikamilifu kutoka ngazi ya matawi hadi Taifa.

TOA MAONI YAKO HAPA

 
Support : Copyright © 2011. HABARILINE - All Rights Reserved